TRC yaongeza safari za SGR baada ya usumbufu kwa abiria

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanzisha safari za ziada za Treni ya Reli ya Kisasa (SGR) kwa lengo la kuwahudumia abiria walioathirika na usumbufu wa safari uliotokea jana, Desemba 28, 2025.