TaSUBa, Ubalozi wa India wawaibua ‘wakali’ sanaa ya uchoraji

Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa kushirikiana na ubalozi wa India, umewashindanisha wanafunzi 20 katika sanaa ya uchoraji iliyobeba mada kuu ya uhusiano wa Bahari wa Hindi na tamaduni za nchi ya Tanzania na India.