Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Emmanuel Nchimbi amesema licha ya uwekezaji katika sekta ya uchukuzi kuhitaji gharama kubwa, Serikali imejipanga kikamilifu kuiboresha sekta ya anga kwa lengo la kuongeza mapato ya fedha za kigeni na kuimarisha mchango wake katika uchumi wa Taifa.