Sauti iliyotulia imeondoka, lakini ujumbe wake umebaki
Usiku wa Alhamisi, Februari 19, 2026, Tanzania ilipoteza kitu ambacho hakiwezi kubadilishwa kwa haraka, sauti ya hekima iliyotokana na imani ya kweli, elimu ya kina na uzoefu wa miaka mingi wa kutumikia watu wa Mungu na Taifa zima.