Wananchi Mwanga walalamikia uhaba nyumba za watumishi wa afya

Baadhi ya wananchi wa kata za Kirya, Kilomeni na Lembeni, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro wamelalamikia ukosefu wa nyumba za wahudumu wa afya katika baadhi ya zahanati, hali inayosababisha kukosekana kwa huduma za dharura nyakati za usiku.