Wataalamu wataja sababu za changamoto za afya ya akili kwa wanaume

Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), takriban mtu mmoja kati ya sita hupitia changamoto ya afya ya akili katika maisha yake, huku zaidi ya asilimia 70 ya vifo vinavyotokana na kujiua vikiwa ni wanaume.