Vijana 308 wapewa Sh7 bilioni kutekeleza miradi ya uvuvi

Kwa mujibu wa Nanauka, vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 35 nchini wanakadiriwa kufikia milioni 20.6, sawa na asilimia 34.4 ya idadi ya watu wote, huku takribani vijana milioni moja wakihitimu mafunzo mbalimbali kila mwaka, lakini ni vijana 40,000 pekee wanaopata ajira katika sekta ya umma na wengine 350,000 sekta binafsi.