Uchaguzi wa viongozi wa Serikali na Bunge ni tukio la kisiasa lenye athari za moja kwa moja kwa mustakabali wa fedha na mazingira ya uwekezaji, na hata uchumi kwa ujumla. Ni jambo la kujivunia kuwa kunakuwapo na uchaguzi katika Taifa, na kipindi hiki ni wakati mwafaka wa kusikiliza na kuchambua sera za vyama mbalimbali.