Mahakama ya Rufaa imesimamisha utekelezwaji wa uamuzi na amri ya Mahakama Kuu Kanda ya Musoma, iliyomuamuru aliyekuwa mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara na wenzake kumlipa fidia ya Sh6 bilioni, Eliakim Maswi, ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria.