Vyama vitatu tayari kwa kampeni, kimoja chaahirisha uzinduzi kitaifa

Vyama vitatu, kikiwamo cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Wananchi (CUF) na Chama cha Wakulima (AAFP), leo vinazindua rasmi kampeni zao za uchaguzi mkuu wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika Jumatano, Oktoba 29, 2025, huku chama kimoja kikiahirisha.