Mwamko mkubwa wa Benki Kuu duniani kununua dhahabu kumeyafanya madini hayo kuwa ya pili miongoni mwa rasilimali kubwa zilizohifadhiwa hiyo ni kwa mujibu wa ripoti ya Benki Kuu ya Ulaya (ECB) iliyotolewa Juni mwaka huu. Hata hivyo, wachambuzi wanasema baadhi ya taasisi zinaonekana kuwa karibu kufikia kiwango cha kutosheka.