Mke mbaroni kwa tuhuma kumuua mumewe na kumzika chumbani

Jeshi la Polisi mkoani Geita linamshikilia Martha Japhet (44), mkulima na mkazi wa Kitongoji cha Mzalendo, Kijiji cha Mawemeru, Kata ya Nyarugusu, Wilaya ya Geita, kwa tuhuma za mauaji ya mumewe, Shabani Paschal (55), ambaye pia alikuwa mkulima na mchimbaji wa madini.