IEBC: Naam, tunachukua mboni ya jicho lako; iko sahihi kuliko alama za vidole

IEBC: Naam, tunachukua mboni ya jicho lako; iko sahihi kuliko alama za vidole

HUKU Tume Huru ya Uchaguzi Nchini (IEBC) ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu wa 2027, Wakenya na wanasiasa wameibua masuali kuhusu teknolojia ambayo itatumika kwenye kura hiyo, mojawapo ikiwa ile ambayo inanasa mboni ya jicho. Mnamo Septemba 29, 2025, IEBC ilianza kuwasajili wapigakura ambapo imekuwa ikiwalenga zaidi ya wapigakura wapya milioni 6.3 (wengi wao wakiwa wapigakura vijana) wakilenga kuongeza idadi ya wale ambao wamesajiliwa hadi milioni 28.7 kufikia mnamo 2027. Usajili huo wa wapigakura kwa sasa unaendelea kwenye maeneobunge 278 pamoja na vituo 57 vya Huduma. IEBC pia inatumia vifaa vya kielektroniki pamoja na vingine kuhakikisha kuna usawa katika usajili wa wapigakura. Hata hivyo, teknolojia ambayo inanasa mboni ya jicho imegeuka kuwa gumzo kuu huku baadhi wakipinga kutumika kwake na wengine wakiunga. Kwa mujibu wa Mtaalamu wa Teknolojia katika IEBC, Bw Gedfrey Ngunyi, kunasa mboni ya jicho kunaongezea tu matumizi ya teknolojia ya kielektroniki ambapo pia alama za vidole huchukuliwa. “Mboni ya jicho ya kila mtu ina upekee wake wala si kama alama za vidole ambazo hutofautiana kwa sababu ya kutegemea kazi ambayo kila mtu hufanya,” akasema Bw Ngunyi. Alifichua kuwa teknolojia hiyo itakuwa ikitumika kutambua mpigakura pale ambapo vidole vitakosa kutambuliwa na mashine ya kielektroniki. “Inaruhisiwa kwenye sheria za uchaguzi na itasaidia katika kuhakikisha kuwa kuna uchaguzi ambao una uwazi mkubwa,” akaongeza. Mkurugenzi wa Kitengo cha Kuwaelimisha wapigakura Joyce Ekuam naye alifichua kuwa wapigakura wanaojisajili hunaswa mboni ya jicho kwa hiari yao wala huwa hawalazimishwi. “Ndiyo mfumo huu upo lakini si wa lazima. Iwapo unahisi si sawa, basi unaweza kutambuliwa kielektroniki tu ambayo ni njia ya kawaida. Tunalenga tu kuhakikisha kuwa mchakato wa kuwatambua wapigakura unaimarishwa zaidi,” akasema Bi Ekuam. Mwenyekiti wa IEBC, Bw Erastus Ethekon kwenye mahojiano na Taifa Leo alisema kuwa data za wale ambao mboni za macho yao zimenaswa zitahifadhiwa salama. “Kupata maelezo ya wapigakura kutadhibitiwa na yeyote ambaye atavuruga na kutumia data hiyo vibaya, atachukuliwa hatua kali za kisheria,” akasema Bw Ethekon. Mwenyekiti huyo wa IEBC aliwahakikishia Wakenya na wanasiasa kuwa teknolojia ambayo itatumika katika uchaguzi huo haitavurugwa na itakuwa na uwazi mkubwa. “Mitandao na vyombo ambavyo tutatumia vina viwango vya juu vya usalama. Nawahakikishia Wakenya kuwa tutawajibika kwa kutekeleza jukumu la tume bila hofu yoyote na uchaguzi utakuwa huru na wenye haki,” akasema Bw Ethekon. Kufikisha wapigakura wapya milioni 6.3, IEBC imetekeleza mabadiliko ambapo si lazima Mkenya ajisajili katika kituo kile ambako atapigia kura. Kwa mfano mtu akifanya kazi Nairobi, Mombasa au Nakuru lakini wanataka kupiga kura mashinani, watachagua tu na kupiga kura kutoka mahali popote walipo.

Spika Wetangula aahirisha kikao cha bunge cha asubuhi, akiahidi kutoa tangazo muhimu

Spika Wetangula aahirisha kikao cha bunge cha asubuhi, akiahidi kutoa tangazo muhimu

SPIKA wa Bunge la Kitaifa Moses Wetang’ula ameahirisha kikao cha asubuhi cha Bunge la Kitaifa cha Jumatano, Oktoba 15, 2025. Kwenye hotuba fupi alipoongoza kikao cha asubuhi cha bunge hilo, saa tatu na dakika 59, Bw Weng’ula alitangaza kuwa bunge hilo litafanya kikao baadaye saa nane na nusu alasiri ambapo atatoa tangazo muhimu. “Nikitumia mamlaka yangu kwa mujibu wa Sheria ya Bunge nambari 1, ninaahirisha kikao hiki.  Kikao kitarejelewa saa nane na nusu leo hii (Jumatano) ambapo nitatoa tangazo muhimu kwa wabunge,” Bw Wetang’ula akasema. Spika huyo alisema hayo baada ya uvumi kutanda nchini haswa mitandaoni kuanzia alfajiri Jumatano kwamba Waziri Mkuu wa zamani, Bw Raila Odinga amefariki nchini India ambako alipelekwa kupokea matibabu. Inatarajiwa Spika Wetang’ula atatoa tangazo hilo rasmi kwa wabunge baada ya familia ya Bw Odinga na Rais William Ruto kuthibitisha bahari hizo.

Ruto Signs Eight Bills into Law

Ruto Signs Eight Bills into Law

President William Ruto on Monday assented to eight Bills passed by the National Assembly into law during a ceremony at State House, Nairobi. The newly signed laws include the National Land Commission (Amendment) Bill, 2023, Land (Amendment) Bill, 2024, Wildlife Conservation and Management (Amendment) Bill, 2023, and the Computer Misuse and Cybercrimes (Amendment) Bill, 2024. [...] The post Ruto Signs Eight Bills into Law appeared first on Kahawatungu .

Raila’s Death: Mourners Flock to His Karen and Bondo Homes as IG Kanja Tightens Security

Raila’s Death: Mourners Flock to His Karen and Bondo Homes as IG Kanja Tightens Security

Former Prime Minister Raila Odinga has died in India following a heart attack, officials confirmed on Wednesday. Odinga, 80, passed away while receiving treatment at the Koothattukulam Sreedhareeyam Ayurveda Hospital in Ernakulam, India. According to medical reports, the veteran opposition leader suffered a cardiac arrest during his morning walk and was rushed to the nearby [...] The post Raila’s Death: Mourners Flock to His Karen and Bondo Homes as IG Kanja Tightens Security appeared first on Kahawatungu .